Sijakuita nikuache hapa
Sijakuita uishie hapa
Nilikuita ili ufike mbali
Naam Mbali kuliko hapa
Sijakuita uishie hapa
Nilikuita ili ufike mbali
Naam Mbali kuliko hapa
Waambie watu wangu wajipe moyo
Waambie wasihofu wala kufadhaika
Kwa maana Mimi Naja kuwaokoa
Sitawaacha, Kwa kuwa Mimi ni Mungu wao
Wakati ukiwa mdogo nalikujua,
Wakati ungali kijana nalikutambua,
Maisha yako yapo mikononi mwangu
Ninazihesabu hatua zako zote
Nimepanga kukupa wokovu
Kwa maana mimi ndiye Mungu Niokoaye
Mwanagu, Sikiliza sauti yangu nawe utanufaika…
Tazama nimepnga mambo mengi mema kwako
Naam… Yatakupata mema
Mimi Mungu nimesema
Jipe moyo mwanagu kwa kuwa mimi ni Mungu wako
Hayo yote yatapita, Kama usiku uutanguliavyo mchana
Pambazuko laja na Baraka zako
Naam, Mimi ni Mungu wako
Mimi ni Nuru iangazayo Gizani
Mimi ni Nuru ya njia yenu
Mimi ni Njia ya wokovu wenu
Mimi ni Wokovu wa Maisha yenu
Mimi ni Ndiye kila kitu
Naam… Huyo Ndiyo Mungu Wenu