Ni afadhali kunikubali kuliko kunikataa
Ni afadhali kunikubali mimi, kuliko kunikataa Kwa maana njia zangu ni njema Je, ni kawaida mtu kukataa kitu kizuri na kuchagua kibaya? La, Si kawaida. Kama sio kawaida, wawezaje kunikataa?
Sitanyamaza kamwe
Kwa sababu hiyo, Sitanyamaza kamwe Mpaka haki ipatikane Haki yako ipo Ninayaona yote
Sijakuita nikuache hapa
Sijakuita uishie hapa Nilikuita ili ufike mbali Naam Mbali kuliko hapa
Nalikujua wewe
Wakati ukiwa mdogo nalikujua, Wakati ungali kijana nalikutambua, Maisha yako yapo mikononi mwangu Ninazihesabu hatua zako zote Nimepanga kukupa wokovu Kwa maana mimi ndiye Mungu Niokoaye
Sikia Mwanangu Sikiliza
Sikia MWanangu sikia… Kama vile baba mwema Ampendavyo mwanaye Ndivyo nami nakujali wewe Ninakupenda upeo
Mimi ni Mungu nikupendaye
Nilikupenda na nitazidi kukupenda Kwa maana mimi ni Mungu wako Nikupendaye