Mimi Mungu huwezi kunificha kwa lolote
Mimi ndiye Mungu niliyekuumba
Mimi ndiye niliyekupa uwezo wa kufikiri na kuamua
Je, unazani unaweza kunificha kitu?
Kwa nini unasema neno jema na kunuia neno baya?
Fahamu tuu kwamba ninajua yote.
Mimi ndiye Mungu niliyekuumba
Mimi ndiye niliyekupa uwezo wa kufikiri na kuamua
Je, unazani unaweza kunificha kitu?
Kwa nini unasema neno jema na kunuia neno baya?
Fahamu tuu kwamba ninajua yote.
Mimi ni Mungu wako, ninayafahamu mawazo yako wakati wote.
Acha kuwaza na kunuia kufanya mambo mabaya, Kwa maana Unazuia Baraka na Rehema zako.
Matendo yako yanaongozwa na nia na mawazo yako.
Chunga nia na mawazo yako kwa kuwa ndiyo njia ya kuelekea kwenye matendo mabaya, kama ikiwa mbaya.
Kwa nini unanionea haya?
Kwa nini unaona ugumu kunitaja?
Je, mimi si ndiye niliyefanya haya yote?
Ni afadhali kunikubali mimi, kuliko kunikataa
Kwa maana njia zangu ni njema
Je, ni kawaida mtu kukataa kitu kizuri na kuchagua kibaya?
La, Si kawaida.
Kama sio kawaida, wawezaje kunikataa?