Mwanagu Nisikilize
Rafiki… Sikia sauti yangu na kupokea fundisho langu Kwa maana huo ndio mwelekeo sahihi
Fungua macho yako
Fungua Macho yako uone, Kwa maana niko nawe lakini hunioni Laiti ungetazama… Ungeniona
Kwa nini unaona haya juu yangu?
Kwa nini unanionea haya? Kwa nini unaona ugumu kunitaja? Je, mimi si ndiye niliyefanya haya yote?
Twende tusonge mbele
Nalikuita, Ukaja. Kwa nini unasita sasa? Songa mbele… Mimi ni Mungu wako Nikuongozaye
Ni afadhali kunikubali kuliko kunikataa
Ni afadhali kunikubali mimi, kuliko kunikataa Kwa maana njia zangu ni njema Je, ni kawaida mtu kukataa kitu kizuri na kuchagua kibaya? La, Si kawaida. Kama sio kawaida, wawezaje kunikataa?
Sijakuita nikuache hapa
Sijakuita uishie hapa Nilikuita ili ufike mbali Naam Mbali kuliko hapa