Mimi Ndimi Mimi
Mimi ni Nuru iangazayo Gizani
Mimi ni Nuru ya njia yenu
Mimi ni Njia ya wokovu wenu
Mimi ni Wokovu wa Maisha yenu
Mimi ni Ndiye kila kitu
Naam… Huyo Ndiyo Mungu Wenu
Mimi ni Nuru iangazayo Gizani
Mimi ni Nuru ya njia yenu
Mimi ni Njia ya wokovu wenu
Mimi ni Wokovu wa Maisha yenu
Mimi ni Ndiye kila kitu
Naam… Huyo Ndiyo Mungu Wenu
Wewe ni Taa, Taa imulikayo Gizani
Wenzio wako gizani, wewe ndio wa kuwaonyesha njia
Mimi ni mwanga, Naam wewe upo na mimi
Wamulike… Wajione
Wamulikie… Wanifuate
Kwa maana nawapenda wote.
Kwa maana nilivyokupenda wewe, nawapenda wao pia
Kwa nini unanionea haya?
Kwa nini unaona ugumu kunitaja?
Je, mimi si ndiye niliyefanya haya yote?
Fungua Macho yako uone,
Kwa maana niko nawe lakini hunioni
Laiti ungetazama…
Ungeniona
Nilikupenda na nitazidi kukupenda
Kwa maana mimi ni Mungu wako
Nikupendaye
Kama ilivyo kwa mzazi anavyotamani kumfanyia mwanae mambo mazuri, Ndivyo nami ninavyokuwazia wewe
Kabla hujapendwa na mzazi wako, nalikupenda wewe
Naam, ninakuwazia mema na ninalenga kukutendea jambo jema
Njoo mwanagu, njoo nyumbani
Njoo mwanagu, njoo nikupendaye