• Sun. Mar 26th, 2023

Mungu.Me

Ujumbe wa Mungu Kwako

Jipe moyo, Mimi ni Mungu wako

Jipe moyo mwanagu kwa kuwa mimi ni Mungu wako. Hayo yote yatapita, Kama usiku uutanguliavyo mchana.

Mwaliko wa Toba ya Baraka

Mwanagu, acha dhambi zako na unirudie mimi. Ninayafahamu mapungufu yako na madhaifu yako. Tubu kwa moyo wako wote nami nitafanya njia

Mimi ni Mungu Nikuwaziaye Mema

Kama ilivyo kwa mzazi anavyotamani kumfanyia mwanae mambo mazuri, Ndivyo nami ninavyokuwazia wewe Naam, ninakuwazia mema na ninalenga kukutendea jambo jema

Acha kuwaza na kunuia kufanya mabaya

Acha kuwaza na kunuia kufanya mambo mabaya, Kwa maana Unazuia Baraka na Rehema zako. Chunga nia na mawazo yako kwa kuwa ndiyo njia ya kuelekea kwenye matendo mabaya.

Lenga Kutenda mema nami nitakubariki

Nuia kufanya Mambo mema mara zote, nawe utabarikiwa. Kwa maana, ninaangalia nia za moyo wako, kwa kuwa huyo ndiyo wewe.